Wednesday, October 14, 2015

MTIKISIKO UCHUMI SUPERMARKET



HALI yasintofahamu katika kampuni ya Uchumi ya jijini Dar es Salaam inayomilikiwa na wakenya jana ilisababisha kazi kusimama kwa siku nzima baada ya wafanyakazi wake kuutaka uongozi kuwaeleza hatima ya ajira na mafao yao baada ya kampuni hiyo kuonekana kuyumba.
Kutokana na sintofahamu hiyo wafanyakazi na waajiri wa kampuni hiyo juzi walilazimika kulala ofisini baada ya wafanyakazi hao kuwazuia kutokana hadi wapate majibu ya hatima yao.
Waandishi waliwashuhudia wafanyakazi hao na waajiri wakiwa ndani na milango ikiwa imefungwa hakuna anayetoka wala kuingia huku wafanyakazi waliolala nje wakiwapitishia vyakula wenzao chini ya milango pamoja na kuwapa maji yakiwa kwenye chupa zilizowekewa mirija ambayo ilikuwa ikipitishwa sehemu ambazo zilikuwa na uwazi.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mlango kufunguliwa na kuruhusiwa kutoka nje,
Mjumbewa Chama cha Wafanyakazi ambaye pia ni mfanyakazi wa kampuni ya Uchumi, GeofreyMuyenzi, 
alisema kuwa kutokana na kuyumba kwa kampuni hiyo waliwaandikia barua waajiri wao ya kuwataka kuwaeleza hatima yao lakini hawakupatiwa majibu.
Alisema kutokana na madeni iliyonayo kampuni hiyo wamelazimika kuulizia hatima yao na kwamba mpaka leo (jana) hatujapatiwa majibu na badala yake baada ya kikao kilichofanyika dhidi ya Chama cha Wafanyakazi. 
Wizara ya Kazi pamoja na waajiri na wanasheria wa kampuni wameahidi kutoa majibu keshokutwa.
“Madeni katika kampuni hii yamezidi na wasambazaji hawaleti tena mizigo yao huku wengine wameanza kuiondoa pia deni la pango limekuwa kubwa kiasi kwamba tunahisi anaweza kuja kufungia mali zawatu wakati wowote,” alisemaMuyenzi.
Naye Katibu wa Chama cha WafanyakaziWilaya yaTemeke (TUICO), George Namkinga alisema kuwa wamekaa katika kikao na uongozi pamoja na wafanyakazi na kukubaliana kuwa majibu yatapatikana kutoka Nairobi keshokutwa katika kingine kikao kitakachowahusishaTUICO mkoa, Serikali, wanasheria wa kampuni pamoja na wafanyakazi lengo ni ili wafanyakazi wapate kujua hatima yao.
Alisema pia lengo ni kampuni iweze kuendelea ili wafanyakazi waweze kuendelea na kazi lakini iwapo ikishindwa kuendelea ndipo sheria zitachukuliwa ili kuwawezesha kupata hatima yao.
“Kweli kampuni ilisuasua na mishahara ikawa inasuasua pia lakini tumefikia pazuri kutokana na kuwa uongozi umejikomiti kwamba kuna jibu na kule Nairobi wametuma wanasheria na tumeweka makubaliano kisheria hivyo hakuna kitakachoharibika,” alisema Namkinga.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya kampuni hiyo ambazo BLOG HII ilizipata, inadaiwa zaidi ya bilioni nne kutoka kwa watu mbalimbali.
BLO HII  ilimtafuta Meneja wa kampuni hiyo nchini kwa njia ya simu Benard Muthin, kuzungumzia madai hayo alisema kuwa hana mamlaka ya kuzungumzia madai hayo.
“Mimi sina mamlaka ya kuzungumzia madai hayo labda niwatumie namba ya simu ya ofisini ili muwatafute wazungumzaji wanaoweza kuzungumzia madai hayo.