SEKTA
ya kilimo ni moja ya sekta muhimu hapa nchini ambayo hapo zamani tuliita kuwa
ni uti wa mgongo wa uchumi wetu.
Mara
baada ya nchi yetu kupata Uhuru, Serikali ilitoa kipaumbele cha kwanza katika
kuendeleza kilimo kama uti wa mgongo wa uchumi wa nchi.
Kilimo kiliajiri zaidi ya asilimia 90 ya
wananchi wote kwa mazao ya katani, kahawa na pamba yaliongoza kulipatia Taifa
fedha za kigeni taifa hili.
kwa
sasa ajira inayotokana na kilimo imeshuka hadi asilimia 80 tu ya watanzania ambapo pato la
fedha za kigeni kutokana na mazao ya kibiashara limeshuka kutokana na kukosekana mipango na utekelezaji wa sera zinazosimamia sekta hii.
Katika
awamu ya kwanza kumekuwapo kaulimbiu na maazimio mbalimbali kama vile “Chakula ni Uhai”, “Siasa ni Kilimo”,“Kilimo cha Kufa na Kupona”, “Mvua za Kwanza ni za Kupandia” ili
kuhamasisha maendeleo ya kilimo, pamoja na kuhamasisha kilimo cha ujamaa.
Awamu
ya Pili iliongozwa na Rais Ali Hassan Mwinyi ambapo tulishuhudia mageuzi ya
kiuchumi ambayo yalikuwa kichocheo kikubwa katika maendeleo ya kilimo ikiwa ni
pamoja na utekelezaji wa Sera ya Kilimo ya mwaka 1983.
Awamu
ya tatu ya uongozi ilikuwa chini ya Rais Benjamin William Mkapa ambapo katika
awamu hiyo kilimo kilipata msukumo wa kipekee kwa kuonyesha mwelekeo Katika awamu
hiyo kutokana na
utekelezaji
wa Sera ya Taifa ya Kilimo na Mifugo ya mwaka 1997 na uanzishwaji wa Mkakati wa
Kuendeleza Sekta ya Kilimo ulishuhudia kilimo kikikua kutoka chini ya asilimia
3 hadi asilimia 6 kulinganisha na awamu zilizotangulia.
Awamu
ya nne ya uongozi ambayo ipo chini ya Rais Dk. Jakaya Kikwete, licha ya kilimo
kuendelea kupewa kipaumbele kikubwa, kwa kaulimbiu mbadala ya kilimo kwanza pamoja
na utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP) na Programu ya
Mageuzi na Modenaizesheni ya Ushirika (CRMP) ambazo zimekuwa chachu ya kuleta mapinduzi
ya kijani hapa nchini lakini lengo halikutimia ipasavyo kutokana na
Licha
ya hayo Jambo kubwa la kujivunia kutokana na kilimo ni kuwa
kwa
sasa asilimia 95 ya mahitaji ya Taifa ya chakula kinazalishwa hapa hapa nchini
kwa Serikali kuweka mfumo wa kuhifadhi chakula kwa ajili ya matumizi wakati upungufu
unapotokea ili kukabiliana na baa la njaa. Takwimu zinadhihirisha kwamba akiba
ya Taifa ya Chakula imekuwa ikiongezeka kila mwaka na uwezo wa Wakala wa Taifa
wa Hifadhi ya Chakula unatarajia kufikia tani 400,000.
Kwa
takribani miongo mitano na ushei ya Uhuru wa nchi yetu, pamoja na kuwa na
changamoto nyingi za kisiasa, kijamii na kiuchumi, kilimo chetu kimeendelea
kuwa nguzo kuu na mhimili wa kujitoshereza kwa chakula tu.
Lakini
iwapo tutakuwa na uthubutu wa kuwekeza inavyopaswa katika kilimo tutaweza si tu
kujitoshereza kwa chakula bali pia kupiga hatua za maendeleo kwa sekta hiyo
adhimu, pengine kiasi cha kurudisha tija kubwa ya pato la kigeni inayoweza
kupatikana kwa kurekebisha mikakati ya mazao ya kibiashara kwa kulenga mahitaji
ya sasa ya soko.
Kimsingi
baadhi ya maeneo muhimu yanayopaswa kuangaziwa na awamu ya tano ya serikali ili
kukirudishia kilimo hadhi yake kamili ni pamoja na tathmini muafaka ya
kilichosababisha kudorora kwa sekta hiyo, ili kubaini nini kifanyike kiutekelezaji
ili kufikia ufanisi wa hali ya juu.
Mathalan,
baadhi ya maeneo muhimu yanayopaswa kutazamwa upya ni pamoja na upatikanaji nafuu
wa pembejeo ambao umekuwa ukisuasua kutokana na gharama kuwa kubwa
ukilinganisha na uwezo wa wakulima wetu.
Uwekezaji
muafaka wa mbinu za kisasa za kilimo kwa kuzingatia matumizi ya nyenzo, mbolea,
kubaini aina ya mazao yanayofaa kulimwa katika ardhi husika pamoja na kuboresha
weledi wa maafisa ughani katika kusimamia kiklimo cha kimapinduzi,
kitakacholitoa taifa letu katyika kilimo cha mazoea kwa ajili ya chakula lakini
kikakidhi pia mahitaji ya kibiashara na kiuchumi.
Kwa
historia ya sekta hiyo hapa nchini kuna mengi tunayoweza kutohoa kutokana na
utekelezaji wa miaka iliyopita, mojawapo ni kuwepo kwa mashamba ya ushirikika
kwa kuwa kimsingi licha ya mengi kati ya mashamba hayo kufa kifo cha asili
lakini bado vyama vya ushirikika vipo. Ni suala la kugeuza tu mashamba
yaliyokuwa katyika muundo huo hata yaliyomilikiwa na serikali, kuwa mikononi
mwa wakulima lakini msisitizo ukiwekwa katika upatikanaji masoko ya kuuzia
mazao yatakayovunwa.
Hayo
yakitekelezwa vyema dhima nzima ya uwepo wa viwanda ili vitumie ghafi muhimu
inayozalishwa kwa kilimo, ndipo itaweza kutimia kikamilifu kwa kuwa soko la
dunia la kilimo kwa sasa limeegemea bidhaa zitokanazo na kilimo zilizokuwa
tayari kwa matumizi na si ghafi inayopaswa kuandaliwa kuwa bidhaa.
hiyo
mikakati ya serikali ya awamu ya tano iliyojinasibu kufufua viwanda wakati wa
kampeni itatimia si kwa kuangalia upande huo tu, bila kuhusisha kilimo kwa kuwa
ilidhihirika wazi wakati wa awamu ya kwanza zao la pamba lilikuwa na soko kubwa
la ndani kutokana na kuwepo viwanda vingi vya kuzalisha nguo, kabla ya ziada
kuuzwa nje na kutupatia fedha za kigeni.
Kuwekeza
kwenye viwanda sanjari na kilimo kuna faida nyingi kwa kuwa tumezungukwa na
masoko yaliyo tayari kupokea bidhaa zetu katika jumuiya zinazotuzunguka ikiwemo
SADC na EAC anvayo kwa sasa ina soko kubwa zaidi kwa kuwa inajumuisha nchi
tano, tofauti na ilivyokuwa awali ilipoundwa na nchi tatu.
Tukienda
mbali zaidi kuna fursa za kimataifa kama ule mpango wa AGOA ambao bado
unatuwezwesha kupata pato kubwa la kigeni nchini Marekani, bila gharama ya tozo
la ushuru wa kuingiza bidhaa nchini humo.
Na kwa
kuwa kinara wa awamu ya rtanio Raisi Magufuli anatokea katika wizara ya ujenzi
na awali alitumikia uchukuzi na uvuzi, tunaamini akiunganisha vyote hivyo na
kunasibisha kilimo naviwanda uchumi utakuwa kwani bidhaa zinazozalishwa
zinahitaji miundo mbinu bora kufikia walaji wa ndani na nchi jirani…
Lakini
ili kufikia mafanikio ya kiwango cha juu kwa sekta hizo zinazotegemeana kuna
haja ya makusudi ya kutathmini baadhi ya changamoto zilizosababisha kilimo
kidumae zikiwemo ardhi ya kilimo kutotambulika
kisheria hivyo kubadilishwa matumizi, jambo linalozalisha migogoro holela baina
ya wawekezaji na wananchi wazawa waliomilikishwa maeneo kwa njia ya kurithi.
Mabadiliko ya tabianchi yanayosababisha kilimo kushindwa kutoa ajira kutokana na upungufu wa mvua, jangwa na kuongezeka kwa joto duniani.
Ushiriki hafifu wa sekta binafsi katika
kilimo ambapo sekta nyingi zimejikita kuwekeza katika fani nyingine.
Ushiriki hafifu wa vijana katika kilimo ambao ndio mguvu kazi na rasilimali watu
kwa kuwa ndio wenye nguvu na uwezo mkubwa, kukikwepa kilimo kwa kukimbilia mijini kufanya
biashara zisizo endelevi.
Uwezo mdogo wa wakulima
kununua zana bora na pembejeo za kilimo
Miundombinu duni katika
maeneo ya uzalishaji wa mazao ya kilimo
Msukumo wa kuzalisha mazao ya
nishati mbadala na madhara yake unakinzana na lengo kuu la kuzalisha mazao ya
chakula kwa baadhi ya wakulima ambapo wengi huangazia kilimo cha chakula na kuachana na mazao ya biashara.
Gharama kubwa ya ujenzi wa
miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji pamoja na maghara ya kuhifadhia mazao pindi yanapovunwa.
Uvamizi wa visumbufu vya
mimea yanayoshindikana kudhibitiwa ambavyo ni pamoja na wadudu na magonjwa mbalim bali ya mimea.
Elimu duni walionayo wakulima pamoja na wadau wa mbalimbali wa kilimo juu ya masuala ya ushirika pamoja na vyama hivi kukosa mitaji na kubaki vikikopa mazao ya wakulima.
Usimamizi hafifu wa sera
ya soko huru ambapo dhana hiyo imekuwa kinyume na matarajio ya wengi na sasa ni kama soko holela lisilokuwa na mdhibiti.
Idadi ndogo ya wataalam wa
kilimo na ushirika pamoja na maslahi duni ukilinganisha na mazingira wanakohitajika kufanya kazi.
Kukosekana kwa mikopo yenye
masharti nafuu ya kuendeleza kilimo kwa mabenki mengi kukwepa kukopesha sekta
hiyo kwa kuichukulia kuwa Nyanja isiyotabirika katika uwezo wa kurudisha
mikopo.
Kimsingi pia lazima kuwekeza kwa
vivutio vya makusudi vitakavyosababisha nguvu kazi kubwa hususan vijana
kujishugulisha na kilimo kama njia ya kuendesha maisha yao na kubadili mtazamo
mzima juu ya sekta hiyo, kwa kurejesha hamasa za kimatendo zaidi kwa kutumia
mbinu za zamani kwa mabadiliko ya kisasa kuanzia ngazi za awali kabisa za
mafunzo ya vinaja wetu katika ngazi mbalimbali za elimu ili wasikikimbie kilimo
badala yake wavutiwe nacho.
Kwa kutimiza hayo na mengine
muambatano naamini kauli mbiu ya HAPA KAZI TU itajisadikisha ipasavyo kwenye
sekta ya kilimo maana matokeo ya kazi ni tija stahiki.
0762656400 KWA MAWASILIANO