Tuesday, November 10, 2015

NANI KUTWISHWA ZIGO LA KUFUFUA KILIMO NCHINI NA DK. MAGUFULI?



SEKTA ya kilimo ni moja ya sekta muhimu hapa nchini ambayo hapo zamani tuliita kuwa ni uti wa mgongo wa uchumi wetu.
Mara baada ya nchi yetu kupata Uhuru, Serikali ilitoa kipaumbele cha kwanza katika kuendeleza kilimo kama uti wa mgongo wa uchumi wa nchi.
 Kilimo kiliajiri zaidi ya asilimia 90 ya wananchi wote kwa mazao ya katani, kahawa na pamba yaliongoza kulipatia Taifa fedha za kigeni taifa hili.
kwa sasa ajira inayotokana na kilimo imeshuka hadi asilimia 80 tu ya watanzania ambapo pato la fedha za kigeni kutokana na mazao ya kibiashara limeshuka kutokana na kukosekana mipango na utekelezaji wa sera zinazosimamia sekta hii.

Katika awamu ya kwanza kumekuwapo kaulimbiu na maazimio mbalimbali kama vile “Chakula ni Uhai”, “Siasa ni Kilimo”,“Kilimo cha Kufa na Kupona”, “Mvua za Kwanza ni za Kupandia” ili kuhamasisha maendeleo ya kilimo, pamoja na kuhamasisha kilimo cha ujamaa.
Awamu ya Pili iliongozwa na Rais Ali Hassan Mwinyi ambapo tulishuhudia mageuzi ya kiuchumi ambayo yalikuwa kichocheo kikubwa katika maendeleo ya kilimo ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Sera ya Kilimo ya mwaka 1983.
Awamu ya tatu ya uongozi ilikuwa chini ya Rais Benjamin William Mkapa ambapo katika awamu hiyo kilimo kilipata msukumo wa kipekee kwa kuonyesha mwelekeo Katika awamu hiyo kutokana na
utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Kilimo na Mifugo ya mwaka 1997 na uanzishwaji wa Mkakati wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo ulishuhudia kilimo kikikua kutoka chini ya asilimia 3 hadi asilimia 6 kulinganisha na awamu zilizotangulia.

Awamu ya nne ya uongozi ambayo ipo chini ya Rais Dk. Jakaya Kikwete, licha ya kilimo kuendelea kupewa kipaumbele kikubwa, kwa kaulimbiu mbadala ya kilimo kwanza pamoja na utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP) na Programu ya Mageuzi na Modenaizesheni ya Ushirika (CRMP) ambazo zimekuwa chachu ya kuleta mapinduzi ya kijani hapa nchini lakini lengo halikutimia ipasavyo kutokana na

Licha ya hayo Jambo kubwa la kujivunia kutokana na kilimo ni kuwa
kwa sasa asilimia 95 ya mahitaji ya Taifa ya chakula kinazalishwa hapa hapa nchini kwa Serikali kuweka mfumo wa kuhifadhi chakula kwa ajili ya matumizi wakati upungufu unapotokea ili kukabiliana na baa la njaa. Takwimu zinadhihirisha kwamba akiba ya Taifa ya Chakula imekuwa ikiongezeka kila mwaka na uwezo wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula unatarajia kufikia tani 400,000.

Kwa takribani miongo mitano na ushei ya Uhuru wa nchi yetu, pamoja na kuwa na changamoto nyingi za kisiasa, kijamii na kiuchumi, kilimo chetu kimeendelea kuwa nguzo kuu na mhimili wa kujitoshereza kwa chakula tu.
Lakini iwapo tutakuwa na uthubutu wa kuwekeza inavyopaswa katika kilimo tutaweza si tu kujitoshereza kwa chakula bali pia kupiga hatua za maendeleo kwa sekta hiyo adhimu, pengine kiasi cha kurudisha tija kubwa ya pato la kigeni inayoweza kupatikana kwa kurekebisha mikakati ya mazao ya kibiashara kwa kulenga mahitaji ya sasa ya soko.

Kimsingi baadhi ya maeneo muhimu yanayopaswa kuangaziwa na awamu ya tano ya serikali ili kukirudishia kilimo hadhi yake kamili ni pamoja na tathmini muafaka ya kilichosababisha kudorora kwa sekta hiyo, ili kubaini nini kifanyike kiutekelezaji ili kufikia ufanisi wa hali ya juu.
Mathalan, baadhi ya maeneo muhimu yanayopaswa kutazamwa upya ni pamoja na upatikanaji nafuu wa pembejeo ambao umekuwa ukisuasua kutokana na gharama kuwa kubwa ukilinganisha na uwezo wa wakulima wetu.
Uwekezaji muafaka wa mbinu za kisasa za kilimo kwa kuzingatia matumizi ya nyenzo, mbolea, kubaini aina ya mazao yanayofaa kulimwa katika ardhi husika pamoja na kuboresha weledi wa maafisa ughani katika kusimamia kiklimo cha kimapinduzi, kitakacholitoa taifa letu katyika kilimo cha mazoea kwa ajili ya chakula lakini kikakidhi pia mahitaji ya kibiashara na kiuchumi.

Kwa historia ya sekta hiyo hapa nchini kuna mengi tunayoweza kutohoa kutokana na utekelezaji wa miaka iliyopita, mojawapo ni kuwepo kwa mashamba ya ushirikika kwa kuwa kimsingi licha ya mengi kati ya mashamba hayo kufa kifo cha asili lakini bado vyama vya ushirikika vipo. Ni suala la kugeuza tu mashamba yaliyokuwa katyika muundo huo hata yaliyomilikiwa na serikali, kuwa mikononi mwa wakulima lakini msisitizo ukiwekwa katika upatikanaji masoko ya kuuzia mazao yatakayovunwa.

Hayo yakitekelezwa vyema dhima nzima ya uwepo wa viwanda ili vitumie ghafi muhimu inayozalishwa kwa kilimo, ndipo itaweza kutimia kikamilifu kwa kuwa soko la dunia la kilimo kwa sasa limeegemea bidhaa zitokanazo na kilimo zilizokuwa tayari kwa matumizi na si ghafi inayopaswa kuandaliwa kuwa bidhaa.
hiyo mikakati ya serikali ya awamu ya tano iliyojinasibu kufufua viwanda wakati wa kampeni itatimia si kwa kuangalia upande huo tu, bila kuhusisha kilimo kwa kuwa ilidhihirika wazi wakati wa awamu ya kwanza zao la pamba lilikuwa na soko kubwa la ndani kutokana na kuwepo viwanda vingi vya kuzalisha nguo, kabla ya ziada kuuzwa nje na kutupatia fedha za kigeni.

Kuwekeza kwenye viwanda sanjari na kilimo kuna faida nyingi kwa kuwa tumezungukwa na masoko yaliyo tayari kupokea bidhaa zetu katika jumuiya zinazotuzunguka ikiwemo SADC na EAC anvayo kwa sasa ina soko kubwa zaidi kwa kuwa inajumuisha nchi tano, tofauti na ilivyokuwa awali ilipoundwa na nchi tatu.
Tukienda mbali zaidi kuna fursa za kimataifa kama ule mpango wa AGOA ambao bado unatuwezwesha kupata pato kubwa la kigeni nchini Marekani, bila gharama ya tozo la ushuru wa kuingiza bidhaa nchini humo.

Na kwa kuwa kinara wa awamu ya rtanio Raisi Magufuli anatokea katika wizara ya ujenzi na awali alitumikia uchukuzi na uvuzi, tunaamini akiunganisha vyote hivyo na kunasibisha kilimo naviwanda uchumi utakuwa kwani bidhaa zinazozalishwa zinahitaji miundo mbinu bora kufikia walaji wa ndani na nchi jirani…

Lakini ili kufikia mafanikio ya kiwango cha juu kwa sekta hizo zinazotegemeana kuna haja ya makusudi ya kutathmini baadhi ya changamoto zilizosababisha kilimo kidumae zikiwemo ardhi ya kilimo kutotambulika kisheria hivyo kubadilishwa matumizi, jambo linalozalisha migogoro holela baina ya wawekezaji na wananchi wazawa waliomilikishwa maeneo kwa njia ya kurithi.
Mabadiliko ya tabianchi yanayosababisha kilimo kushindwa kutoa ajira kutokana na upungufu wa mvua, jangwa na kuongezeka kwa joto duniani.

 Ushiriki hafifu wa sekta binafsi katika kilimo ambapo sekta nyingi zimejikita kuwekeza katika fani nyingine.

 Ushiriki hafifu wa vijana katika kilimo ambao ndio mguvu kazi na rasilimali watu kwa kuwa ndio wenye nguvu na uwezo mkubwa, kukikwepa kilimo kwa kukimbilia mijini kufanya biashara zisizo endelevi.
              
Uwezo mdogo wa wakulima kununua zana bora na pembejeo za kilimo
 Miundombinu duni katika maeneo ya uzalishaji wa mazao ya kilimo

Msukumo wa kuzalisha mazao ya nishati mbadala na madhara yake unakinzana na lengo kuu la kuzalisha mazao ya chakula kwa baadhi ya wakulima ambapo wengi huangazia kilimo cha chakula na kuachana na mazao ya biashara.

Gharama kubwa ya ujenzi wa miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji pamoja na maghara ya kuhifadhia mazao pindi yanapovunwa.

Uvamizi wa visumbufu vya mimea yanayoshindikana kudhibitiwa ambavyo ni pamoja na wadudu na magonjwa mbalim bali ya mimea.

Elimu duni walionayo wakulima pamoja na wadau wa mbalimbali wa kilimo juu ya masuala ya ushirika pamoja na vyama hivi kukosa mitaji na kubaki vikikopa mazao ya wakulima.
Usimamizi hafifu wa sera ya soko huru ambapo dhana hiyo imekuwa kinyume na matarajio ya wengi na sasa ni kama soko holela lisilokuwa na mdhibiti.
Idadi ndogo ya wataalam wa kilimo na ushirika pamoja na maslahi duni ukilinganisha na mazingira wanakohitajika kufanya kazi.
Kukosekana kwa mikopo yenye masharti nafuu ya kuendeleza kilimo kwa mabenki mengi kukwepa kukopesha sekta hiyo kwa kuichukulia kuwa Nyanja isiyotabirika katika uwezo wa kurudisha mikopo.

Kimsingi pia lazima kuwekeza kwa vivutio vya makusudi vitakavyosababisha nguvu kazi kubwa hususan vijana kujishugulisha na kilimo kama njia ya kuendesha maisha yao na kubadili mtazamo mzima juu ya sekta hiyo, kwa kurejesha hamasa za kimatendo zaidi kwa kutumia mbinu za zamani kwa mabadiliko ya kisasa kuanzia ngazi za awali kabisa za mafunzo ya vinaja wetu katika ngazi mbalimbali za elimu ili wasikikimbie kilimo badala yake wavutiwe nacho. 
Kwa kutimiza hayo na mengine muambatano naamini kauli mbiu ya HAPA KAZI TU itajisadikisha ipasavyo kwenye sekta ya kilimo maana matokeo ya kazi ni tija stahiki.
0762656400 KWA MAWASILIANO