Monday, July 6, 2015

TTCL KUPELEKA MAWASILIANO KWA WATEJA WALIO NJE YA MKONGO



KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL), imeanza kuwawezesha wateja wake yakiwamo makampuni, taasisi na ofisi za Serikali kupata mawasiliano ya intaneti sehemu zilizo mbali na njia ya mkongo wa Taifa wa Mawasiliano.

Taarifa hiyo ilitolewa na Ofisa Mtatuzi wa Masuala ya Kiufundi wa TTCL, Fredrick Bernad alipokuwa akizungumza katika Maonesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam maarufu kama maonyesho ya Sabasaba.
Kwa mujibu wa Benard, teknolojia hiyo ni mpya na ni muhimu kwa kampuni na wateja wengine kwani ni bora na ni ya uhakika kwa mawasiliano.
“Mbali na mawasiliano ya intaneti, wateja wanaweza pia kupata huduma ya kupata mawasiliano ya shughuli za kiofisi zaidi ya mbili ambazo zipo maeneo tofauti na kushirikiana kwa taarifa na mifumo ya kompyuta iitwayo Mpls Vpn.

“TTCL iliamua kuleta huduma hiyo kutokana na mahitaji makubwa ya matumizi ya intaneti kwa shughuli za maendeleo kwani kuna maeneo ambayo awali yalihitaji huduma ya mkongo lakini kutokana na umbali pamoja na gharama imekuwa ngumu kuwapelekea huduma.

No comments:

Post a Comment