Msanii wa
Vichekesho Ismail Makombe maarufu Baba Kundambanda afariki dunia asubuhi ya leo.
Kwa mujibu
wa taarifa kutoka kwa ndugu wa karibu zinasema Kundambanda amefariki alfajiri
ya leo mjini Masasi kutokana na maradhi ya kifua.
“Juzi alibanwa
na kifua akaenda mwenyewe hospitali huku akiendesha gari, akapatiwa matibabu na
jana kuanzia mchana ndipo hali ilipobadilika na hatimaye leo alfajiri kufariki
dunia,” kilisema chanzo hicho.
Chanzo hicho
kilisema kuwa taratibu za mazishi zinaendelea nyumbani kwake Masasi
FICHUA inawatakia subira wafiwa wote na mungu aipumzishe roho ya marehemu pema peponi. amen
No comments:
Post a Comment