Friday, July 22, 2016

mchekeshaji mwingine afariki dunia



Msanii wa Vichekesho Ismail Makombe maarufu Baba Kundambanda afariki dunia asubuhi ya leo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa ndugu wa karibu zinasema Kundambanda amefariki alfajiri ya leo mjini Masasi kutokana na maradhi ya kifua.
“Juzi alibanwa na kifua akaenda mwenyewe hospitali huku akiendesha gari, akapatiwa matibabu na jana kuanzia mchana ndipo hali ilipobadilika na hatimaye leo alfajiri kufariki dunia,” kilisema chanzo hicho.
Chanzo hicho kilisema kuwa taratibu za mazishi zinaendelea nyumbani kwake Masasi
FICHUA inawatakia subira wafiwa wote na mungu aipumzishe roho ya marehemu pema peponi. amen
 

No comments:

Post a Comment