BENDI ya
Msondo Ngoma imewataka mashabiki na wapenzi wa muziki wa dansi nchini
kujitokeza katika tamasha la siku ya Familia litakalofanyika leo katika ukumbi
wa DDC Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Meneja wa
bendi hiyo, Said Kibiriti aliliambia DIMBA kuwa lengo ni kuwa na wasaa wa
kukutana na mashabiki wao ikiwa ni pamoja na kubadilishana mawazo na kuichangia
bendi hiyo ili iweze kufanya vema.
Alisema
onesho hilo litawakumbusha mashabiki kuwa bendi ipo na inaendelea kufanyakazi
vizuri.
“Katika
onesho hilo tunatarajia kutambulisha nyimbo mpya mbili ambazo ni ‘Masimango’
ukiwa ni utunzi wa Edo Sanga na ‘maana ya ndoa iko wapi’ ukiotungwa na
mwanamuziki Athumani Kambi,” alisema Kibiriti.
mwisho
No comments:
Post a Comment