Friday, July 22, 2016

SIKU YA FAMILIA YA MSONDO JUMAPILI



BENDI ya Msondo Ngoma imewataka mashabiki na wapenzi wa muziki wa dansi nchini kujitokeza katika tamasha la siku ya Familia litakalofanyika leo katika ukumbi wa DDC Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Meneja wa bendi hiyo, Said Kibiriti aliliambia DIMBA kuwa lengo ni kuwa na wasaa wa kukutana na mashabiki wao ikiwa ni pamoja na kubadilishana mawazo na kuichangia bendi hiyo ili iweze kufanya vema.
Alisema onesho hilo litawakumbusha mashabiki kuwa bendi ipo na inaendelea kufanyakazi vizuri.
“Katika onesho hilo tunatarajia kutambulisha nyimbo mpya mbili ambazo ni ‘Masimango’ ukiwa ni utunzi wa Edo Sanga na ‘maana ya ndoa iko wapi’ ukiotungwa na mwanamuziki Athumani Kambi,” alisema Kibiriti.
mwisho

No comments:

Post a Comment