Tuesday, May 19, 2015

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM WAFANYA MGOMO BARIDI



UONGOZI wa Serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam(DARUSO), umeiomba serikali kuacha urasimu wa kuwalipa fedha za mikopo na badala yake watekeleze kama walivyokubaliana katika mikataba yao.
Akizungumza jana wakati wakifanya mgomo baridi kushinikiza kulipwa fedha zao za kujikimu,Waziri wa Mikopo ya wanafunzi wa chuo hicho, Shitindi Venance alisema inashangaza kuona baadhi ya viongozi wa serikali ambao wamekuwa wakitumia mabilioni ya fedha wakidai ni ya mboga wakati wao wakishindwa kutekelezewa ahadi za mikataba yao.
“Nchi hii imefikia pabaya, inashangaza Waziri anayekumbwa na kashfa anatangaza kuwa bilioni 10 ni fedha za mboga wakati sisi tunadai bilioni 2.8 za kujikimu kwa wanafunzi 6120 wameshindwa kutulipa jambo ambalo linatujengea taswira mbaya,” alisema Venance.
Venance alisema serikali iache kufanya kazi kwa mazoea kwa kusubiri shinikizo la migomo ndipo watekeleze majukumu yao kwani wanajijengea muundo mbaya.
Alisema viongozi wengi walioko madarakani wanatumia vibaya nyazifa na fedha zao kuwalaghai wanafunzi wa kike nao kwa shida walizonazo wanakubali kuingia kwenye mitego yao.
“Wasifikiri hatuoni wanavyokuja na mashangingi kuwalaghai dada zetu wakati hawataki kuwapi fedha zao kwa wakati wawalipe ili wasiingie vashawishini,” alisema venance.
Alisema waliingia mkataba na Bodi ya Mikopo kuwa kila baada ya wiki nane watakuwa wanawaingizia 450,000 fedha za kujikimu lakini hadi sasa wiki ya 11kiongozi yeyote aliyelizungumzia hilo.
 Aliongeza kuwa baada ya kuona kuwa fedha hazijaingizwa walienda hadi Bodi ya Mikopo ambao nao walidai hawajapewa fungu hilo na walipoenda Wizara ya Fedha bado hakukuwa na jibu la kueleweka.
“Tunaupongeza uongozi wa Chuo ambao umeahidi kutukopesha shilingi 20,000 ili kupunguza makali japokuwa fedha hizo hatukuzipokea kwa kuwa hazitosherezi mahitaji yetu,” alisema.
 Alisema wamekuwa wakisoma kwa shida kwa muda mrefu ambapo  hata mwaka jana walienda kufanya mafunzo kwa vitendo(field attachment)bila kulipwa fedha hadi waliporejea.
“Mwaka huu tunatangaza kabisa kama fedha za ‘field’ hakuna hatuendi,” alisema.
Alisema Serikali inawafundisha vibaya kuwa bila kuiadhibu haitekelezi jambo.
“Baada ya leo (jana) kuanza kushinikiza mgomo kwa kukataa kuingia darasani, tumeambiwa lazima ziingie… nasi hatulali leo kama fedha hazijaingia tutakesha,” alisema.
BLOG hii ilifika chuoni hapo na kuwakuta wanachuo wakiwa wamekusanyika eneo moja huku wakiwa wametulia wakisubiri maagizo ya viongozi ambao walikuwa wakihaha huku na kule kujua hatma yao bila ya kuleta taharuki ndani ya chuo.
Kwa upande wake Msemaji wa Bodi ya mikopo ya Wanafunzi, Cosmas Mwaisobwa alisema madai ya wanafunzi hao yanashughulikiwa na si chuo hicho tu.
“Ni kweli baadhi ya wanafunzi wanadai na madai yao yanashughulikiwa na si chuo hicho tu kuna vyuo vingi ambavyo vina madai kama hayo

No comments:

Post a Comment