VIJANA wa
wilaya ya Rufiji wameamua kutoa elimu ya mpiga kura kwa wananchi hasa kipindi
cha kura za maoni ili kujenga uelewa kwa wananchi hao .
Wakizungumza jijini Dar es Salaam kwa nyakati tofauti vijana hao walisema
wameamua kutoa elimu hiyo ili kuubadilisha mfumo uliopo hasa ndani ya Chama cha
Mapinduzi(Ccm) ambao unawanyima haki ya kuchagua kiongozi bora.
Mmoja kati
ya vijana hao,Juma Kiholobele alisema mfumo uliopo unasababisha watu wenye fedha
kuwa ndio wenye haki ya kuwa viongozi.
“Tunaenda
kuwaeleza wenzetu wasiojua kabisa, wanaojua kidogo na wanaojua sana kuwa lazima
mfumo urudi kama ulivyoasisiwa ambapo tulikuwa tukiangalia uwezo wa mtu katika
uongozi,” alisema Kiholobele.
Alisema
mfumo wa kugawa fedha kipindi cha uchaguzi unawanyima wananchi haki ya
kusikiliza sera na malengo ya mgombea.
“Tutapambana
na mfumo uliopo ambao fedha zinatumika kama raslimali ya kupata uongozi ambapo
mamlaka yanabaki kwenye familia chache zenye kipato,” alisema Kiholobele.
Alisema
mfumo huo unasababisha watu wenye fedha kuwa wizi kwa kuwa itabidi warudishe
mitaji yao(fedha) waliyotoa kipindi cha uchaguzi hivyo kurudisha maendeleo ya
nchi nyuma.
Alisema
mabadiliko yapatikane ndani ya CCM ikishindikana watayatafuta nje.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa Uvccm wilayani Rufiji, Shabani Matwebe alisema atahakikisha
wanachama, viongozi na mashabiki wa CCM wanafuata katiba na kanuni za chama
hicho katika kupata wagombea.
“Vijana
tuone kama tumechelewa kuubadili mfumo huu kwani katiba na kanuni za CCM katika
kupata wagombea tunazijua na ni lazima sasa tuzitumie na si kusubiri nani ana
fedha nyingi mwaka huu,” alisema Matwebe.
Alisema kura
za maoni mwaka huu ndani ya chama hicho zitakuwa za ushindani kama CHADEMA na
CCM kutokana na watu kuelimika kupitia wao.
Nae
mwanachama wa ccm, Jamvi Magawa alisema rushwa ndani ya CCM ndiyo chanzo cha
tatizo la ukosefu wa maadili ndani ya chama hicho.
“Kwa sababu
ya rushwa tumeendelea kuonewa na kunyanyaswa kwani hatuna mamlaka ya kumuuliza
kiongozi ambae tulimchagua kwa wingi wa fedha zake kwa sababu tulikula 15,000
zake mwaka 2010,” alisema Magawa.
Alisema
viongozi wanapokuwa vipofu kuona matatizo ya wananchi wao, wananchi watakuwa
viziwi hawatawasikiliza viongozi wao.
No comments:
Post a Comment