WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salam (UDSM), wameiomba serikali
kuhakikisha inaweka mfumo madhubuti wa kuandikisha wanafunzi kwenye daftari la
Kudumu la Wapiga kura ili haki yao kikatiba itekelezeke.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Waziri wa
Mikopo wa Serikali ya Wanafunzi (DARUSO), Shitindi Venance alisema, hadi sasa
hakuna utaratibu wowote wa wao kuandikishwa katika daftari hilo jambo ambalo
linaonyesha kuwanyima haki yao ya msingi.
“Sisi kama wanavyuo na kila aliyepo chuoni hapa ni mtu mzima
ametimiza miaka 18, lakini kwa utaratibu uliopo inaonyesha dhahiri wanataka
kutunyima haki yetu ya kuwachangua viongozi tunaoona wataleta mabadiliko nchini.
“Tumeamua kutoa ombi hili baada ya kuona utaratibu wa
kuandikisha ukiendelea kufanyika katika majimbo yetu wakati sisi tupo chuoni tukiendelea
na masomo na hadi sasa hatujapewa utaratibu wa kuandikishwa katika vyuo,” alisema
Venance.
Venance alisema ni vyema serikali ikaona haja ya kufungua
matawi katika vyuo mbalimbali nchini na kuandikisha wanafunzi katika daftari
hilo ili wapate haki ya kumchagua kiongozi wanayemhitaji.
Alisema inasikitisha sana wao kukosa haki hiyo hadi sasa kwani
vijana ndiyo wenye kuleta changamoto ya kupata viongozi wenye manufaa ambao wako
tayari kuleta mageuzi ya kiuchumi katika majimbo yao.
“Tunaomba Serikali iliangalie kwa umakini suala hili kwani
sisi ndiyo wenye uwezo wa kuwaelimisha wananchi vijijini kiongozi yupi anafaa
hasa ukizingatia maeneo hayo baadhi yao hawana uelewa wa yupi anafaa kuwa
kiongozi bora,” alisema Venance.
Alisema
mzalendo wa kweli anaheshimika kwa elimu yake na si kumfundisha mtu uzalendo
kwa kumpeleka jeshini ambapo aliiomba serikali kuwaelewa katika hilo
No comments:
Post a Comment