Tuesday, May 19, 2015

GONJWA LA AJABU LAIBUKA



WIZARA ya Afya na Ustawi wa Jamii imetuma wataalamu katika mkoa wa Simiyu ambako kumeripotiwa kuwepo na ugonjwa unaosababisha watu kuongea ovyo.
                         
Ugonjwa huo uliibuka mwanzoni mwa mwezi huu wilayani Meatu mkoani Simiyu na kusababisha watu 80 kuugua.

Akizungumza jana, Msemaji wa wizara hiyo, Nsachris Mwamwaja, alisema wataalamu hao walitumwa wiki iliyoita na wanaendelea na uchunguzi ili kubaini ni aina gani ya ugonjwa.

“Tayari kuna sampuli zimeletwa Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi...unaweza ukawa unaongea ovyo lakini wakachukua sampuli za damu hivyo tusubiri majibu,” alisema Mwamwaja.

Alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa watu hao pia walikuwa na magonjwa mengine ya kuhara na kutapika.

Mbali na kuongea ovyo, watu wanaokumbwa na ugonjwa huo huishiwa nguvu na kuumwa kichwa.

Baadhi ya waathirika waliofikishwa katika vituo vya afya walipimwa na kubainika hawana ugonjwa wowote na badala yake kubaki wakiweweseka.

Mkuu wa wilaya ya Meatu, Erasto Sima alisema kuwa ugonjwa huo ulizikumba kata za Mwandoya, Mwabusalu, Lingeka, Mwakisandu, Tindabuligi na Lubiga.


Kulingana na Mkuu huyo wa Wilaya, baadhi ya wagonjwa wamekuwa wakiishiwa nguvu, kuongea maneno yasiyoeleweka, kuwapiga wenzao, kugongwa na kichwa, kutokwa na mafua na kukohoa kikohozi kikavu.













No comments:

Post a Comment